TUENDELEE KUTUMAINI

Ni nani kati ya wana wa Israeli waliotekwa angefikiri kwamba wangeiona tena Yerusalemu? Hakuna.
Tumaini lote likakatizwa, wakakumbuka Sayuni na kulia.

« Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni. Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu. Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni. Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni? »(Zaburi 137:1-4)

Sisi pia tuna kumbukumbu nzuri tulizowahi kuishi nyumbani au kwingineko, na kumbukumbu nyingine tulizokuwa nazo zamani, huzuni zinazobadilika mioyoni mwetu, na hata tunalia kwa sababu tunafikiri kwamba hatutaziona tena.
Lakini tunakuwa tunajidanganya kama wale wana wa Israeli waliokuwa wamekata tamaa na kulia kana kwamba hawataiona tena Yerusalemu.
Kutukanwa, kudhalilishwa, na kudhihakiwa kama wana wa Israeli kusitufanye tukate tamaa, bali tuwe na tumaini kwamba mipango ya Mungu ni nzuri kwetu, kwamba tutarudishiwa yale ambayo Shetani alitunyang’anya na kwamba tutakuwa na nyakati nzuri kama zile tuliokuwa tunaishi.
Baada ya yote, « kuna tumaini kwa mti: Ukikatwa utachipuka tena, wala machipukizi yake mapya hayatapungua. »(Ayubu 14:7)
Basi tuendelee kutumaini!

OMBI:
Bwana Mungu wetu, utuwezeshe kuweka tumaini.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☏: +250730900900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *