TUSIJIAMINI SANA

Tunaposhauriwa tusimwamini mtu yeyote, pia tunashauriwa tusijiamini sana, kwa sababu jinsi wengine wanavyofanya makosa au kushindwa kutimiza ahadi zetu, ndivyo sisi pia tunavyofanya.

“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe.”(Mithali 3:5)

Kujiamini sio jambo baya, ni jambo jema.
Unapoamini kuwa unaweza kufanya jambo, ni rahisi kulifanya kuliko unapotilia shaka au kudharau uwezo wako.
Ubaya ni kujiamini kupita kiasi.
Lakini tusipoweka tumaini letu kwa Bwana Mungu, mfano bora wa kujiamini unaweza kuwa « kuwa wenye hekima machoni petu wenyewe » na « kutegemea akili zetu wenyewe ».
Sasa tunajiweka mahali pa juu panapostahili Mungu pekee.
Hata hivyo Biblia inatuambia:
« Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga. »(Mithali 28:26)

Hatupaswi kujitegemea wenyewe, kwa sababu tunahitaji mtu mwenye hekima zaidi, mwenye nguvu na mkamilifu zaidi. Huyo ndiye Bwana Mungu wetu.

OMBI:
Bwana Mungu wetu, utujalie tusijiamini kupita kiasi.
Ni katika jina la thamani la mtoto wako Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☏: +250730900900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *