ALIFANYA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA !

Sulemani ambaye alipokea kutoka kwa Mungu zawadi ya hekima na ambaye alikuwa na baba yake Daudi kama mfano kuhusu uhusiano na Mungu, alifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana.

« Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake. »(1 Wafalme 11:6).

Ni nini kilitokea kwamba Sulemani alikuja kufanya maovu machoni pa Mungu wakati alikuwa na hekima?

1. Moyo wake uligeuzwa na wanawake:
Sulemani alipenda wanawake wengi. Alikuwa na wake mia saba za kifalme pamoja na masuria mia tatu. Wanawake hawa wote walimfanya Sulemani amwache Mungu.(Soma 1 Wafalme 11:3-4)
Yeyote anayejiingiza katika upendo wa wanawake bila shaka amedhoofika kiroho.

2. Hakubaki kumsikiliza Mungu:
Sulemani alipaswa kutumia maneno yake mwenyewe ya hekima ikiwa angedumu katika uhusiano na Mungu.
Tusipomsikiliza Mungu, hatuwezi kukaa katika ukweli. Na kupotea kutoka kwa ukweli ni kufanya maovu mbele ya Mwenyezi Mungu.

OMBI:
Baba yetu uliye mbinguni, utusaidie tusitende maovu kamwe machoni pako.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☏: +250730900900
KIGALI-RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *