JE, WEWE NI KIUMBE KIPYA ?

Biblia inasema kila amwaminiye Kristo anakuwa kiumbe kipya. Na mabadiliko lazima yafanyike katika mawazo na matendo yake.

“Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.”(2 Wakorintho 5:17)

Kwa hivyo, ikiwa unasema uko ndani ya Kristo, ni nini kimebadilishwa katika maisha yako?
Kwa kawaida, mabadiliko lazima yatendeke katika maisha yako “kwa kufanywa upya na Roho Mtakatifu.”(Tito 3:5)
Mawazo yetu na kazi zetu, lazima zifanane na za Kristo.
“Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu.”(Wafilipi 2:5)
« Mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.”(Wafilipi 4:8)
Ni sawa na matamanio yetu, lazima asiwe na hamu na mali ya ulimwengu.
Ni lazima “ukafuate haki, utauwa, imani, upendo, saburi, upole.”(1 Timotheo 6:11)

OMBI:
Baba wa Mbinguni, tupe urahisi katika mabadiliko ambayo Roho Mtakatifu anafanya katika maisha yetu.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☎: +250 730 900 900
KIGALI-RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *