MUNGU ANASIKIA KILIO CHETU !

Tunapokuwa katika dhiki au katika maisha duni, tunaweza kuhisi kuachwa na kusahauliwa na Mungu.
Lakini ukweli ni kinyume cha kile tunachofikiri au kuhisi.

« Maana hakulidharau teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake, Bali alipomlilia akamsikia. »(Zaburi 22:24)

Vyovyote hali zetu Mungu husikia kilio chetu.
“Yesu, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.”(Waebrania 5:7)
Kwa hiyo ina maana kwamba kumcha kwa Mungu kunabomoa kuta zote na mwingiliano wote ambao ungeweza kumzuia Mungu kusikia kilio chetu.
Ikiwa ndivyo, basi kwa nini tusitafute kuwa wacha Mungu?

OMBI:
Baba yetu uliye mbinguni, utujalie tuwe wachamungu.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☏: +250730900900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *