UPENDO WA MUNGU WATOSHA

Kuna watu hukata tamaa wakati wengine hawawapendi au hawawajali.
Na bado, upendo wa Mungu, unaopita upendo wote wa kibinadamu na ufikirio, unatutosha.

« Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. »(Yohana 3:16)

Watu si lazima watupende, hata hawapaswi kutuheshimu pia. Anayepaswa kutupenda na kutuheshimu ni Mungu wetu.
Mungu anatupenda na anatuheshimu kwa sababu anajua thamani yetu kwa kuwa alituumba kwa mfano wake na kwa kumtoa mtoto wake kuwa dhabihu kwa ajili yetu.

Kwa hiyo tusiwe na wasiwasi kwamba kuna watu ambao hawapendi au hawatuheshimu. Hayo, hayo yatajibiwa na Mungu.
Kutoka kwetu, tuwapende na tuwaheshimu wote.

OMBI:
Baba yetu uliye mbinguni, utujalie turidhike na upendo wako.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☎: + 250 730 900 900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *