KUMBUKA !

Watu wa Israeli kwa hakika waliona uweza wa Mungu, kwa njia ya ajabu sana ambayo aliwatoa kutoka Misri, akiwakomboa kutoka kwa mkono wa Farao, na kulishwa jangwani. Na Musa anawaalika watu wasisahau haya yote, ili wasigeuke kutoka kwa Mungu.

« Kumbuka sana Bwana, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote; uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako. »(Kumbukumbu la Torati 7:18-19)

Bwana anataka sisi pia tukumbuke yale ambayo ametufanyia, ili tubaki kushikamana Naye, tubaki tukiwa na furaha daima na katika mtazamo wa shukrani. Kwa sababu, katika maisha yetu pia, Amefanya mambo mengi ya ajabu! Tukumbuke hilo.

OMBI:
Baba yetu uliye mbinguni, utujalie kukumbuka wema wako daima ili tusije tukakuacha kamwe.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☏: +250730900900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *