MUNGU AKINIJALIA !

Sote tumekatishwa tamaa na ahadi zilizovunjwa. Na kwa hakika, pia ilitokea kwetu kutoheshimu ahadi zetu bila ya mapenzi yetu. Hiyo ina maana kwamba kila kitu kinategemea mapenzi ya Mungu.

Alipotaka kuondoka Efeso, mtume Paulo aliwaambia waandamani wake hivi:
“Nitarejea kwenu tena, Mungu akinijalia.” Akatweka, akatoka Efeso.(Matendo ya Mitume 18:21)

Paulo alikuwa sahihi, kwa sababu hatuwezi kufanya lolote isipokuwa Mungu anataka tufanye.
Ajali, ugonjwa, kufungwa gerezani, kufukuzwa kazi, kifo na hali nyinginezo zinaweza kuingilia kati kutuzuia kufanya yale tuliyopanga au kuahidi kufanya.
Bila shaka, ni lazima tuombe kwa ajili ya mipango yetu yote, lakini tunapaswa kujua kwamba mipango yetu itatimizwa tu “Mungu akitujalia.”(Waebrania 6:3)
Hivyo ni vyema tukawa na tabia ya kusema kila mara « MUNGU AKITUJALIA », tunapoahidi au kupanga kufanya jambo fulani.(Soma Yakobo 4:14-15)
Na MUNGU AKITUJALIA, hakuna kinachoweza kutuzuia.

OMBI:
Baba yetu uliye mbinguni, utujalie tuwe chini ya mapenzi yako daima.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☎: +250 730 900 900
KIGALI-RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *