TOWA KWA MOYO WA KUPENDA

Biblia inatuhimiza sikuzote tuwe tayari kuchangia kwa moyo wote kwa ajili ya kazi ya Bwana.

« Wakaja kila mtu ambaye moyo wake ulimhimiza, na kila mtu ambaye roho yake ilimfanya kuwa apenda, nao wakaleta sadaka za kumpa Bwana, kwa kazi ya hema ya kukutania, na kwa utumishi wake, na kwa hayo mavazi matakatifu. »(Kutoka 35:21).

Sheria za matoleo kwa ajili ya ujenzi wa hema ya kukutania zilikuwa wazi: Ni wale tu waliochochewa na moyo na kuchochewa na nia njema ndio pekee wanaoleta matoleo huko.
Hata kama matoleo hayo yalikuwa ya hiari, kila mtu angetoa kile alicho nacho.(Soma Kut 35:22-28)
« Wana wa Israeli wakaleta sadaka za kumpa Bwana kwa moyo wa kupenda; wote, waume kwa wake, ambao mioyo yao iliwafanya kuwa wapenda kuleta kwa hiyo kazi, ambayo Bwana aliamuru ifanywe kwa mkono wa Musa. »(Kutoka 35:29)

Makanisa yetu mbalimbali yana wito wa kazi ya Mungu, ni kwa sababu hiyo kila Mkristo mwema anapaswa kuhuishwa na mapenzi mema ili kutoa mchango wake katika ujenzi wa kanisa lake.
Kuna wengine hufanya hivyo ili kujionyesha au kukubalika kanisani, wengine hufanya hivyo kwa woga au shinikizo la wachungaji wa kanisa, lakini sisi tunapashwa fanya hivyo kwa dhati.
Hebu mioyo yetu iwe tayari kila wakati kutoa mchango wowote katika ujenzi wa kanisa.

OMBI:
Baba yetu uliye mbinguni, utujalie kuwa tayari kusaidia kujenga kanisa letu.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☎: + 250 730 900 900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *