TUSIWAKWAZE WENGINE

Mtume Paulo anatuambia kwamba tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiwakwaze wengine.

“Mtu asitie kitu cha kumkwaza ndugu au cha kumwangusha.”(Warumi 14:13)

Ndiyo, tuna haki ya kufurahia uhuru wetu katika Kristo, lakini pamoja na uhuru huo huja wajibu wa kuwalinda wale walio karibu nasi ambao wana shaka juu ya uhuru huo.
Tukitenda vibaya, tutakuta tumewakwaza kiroho.
Ndiyo maana, kama Wakristo, tumekatazwa kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuwafanya ndugu na dada zetu katika Kristo wajikwae kwa kiroho. Na kujikwaa kunaweza kusababisha mtu kuanguka kiroho, au kuharibu au kudhoofisha imani yake.
Katika mambo yote, somo muhimu ni “kujitahidi kufanya mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana.”(Warumi 14:19). Kwa njia hii, Mungu hutukuzwa, waumini wanajengwa, na ulimwengu unaona ndani yetu “haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu”(Warumi 14:17).

OMBI:
Bwana Mungu wetu, utusaidie tusiwakwaze wengine kamwe.
Ni katika jina la thamani la mwanao Yesu Kristo tunaomba, Amina.

THE LION OF JUDAH MINISTRY IN THE WORLD©
thelionofjudahmission@gmail.com
☏: +250730900900
KIGALI – RWANDA

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *